JamiiCanada
Mshukiwa wa shambulio la Vancouver afikishwa mahakamani
28 Aprili 2025Matangazo
Mshukiwa huyo aliyefahamika kuwa na historia ya matatizo ya afya ya akili, alitambuliwa kama Kai-Ji Adam Lo, mwenye umri wa miaka 30 na mkazi wa Vancouver ambaye alishtakiwa kutenda makosa hayo kwa makusudi bila hata hivyo kufahamu sababu iliyopelekea kitendo hicho.
Soma pia: Watu kadhaa wauawa baada ya gari kuvurumishwa katikati ya umati Canada
Siku ya Jumamosi, gari ilivurumishwa katikati ya umati wa watu waliokuwa wakihudhuria tamasha la mitaani la Kifilipino linalojulikana kama "Lapu Lapu" katika mji wa magharibi wa Vancouver nchini Canada.