MigogoroMashariki ya Kati
Huduma za kiutu hatarini kuporomoka kabisa Gaza
2 Mei 2025Matangazo
Taarifa ya shirika hilo imesema bila ya misaada kuanza haraka kuingizwa Gaza, kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu itashindwa kupata chakula, dawa na vifaa vingine vya kuokoa maisha vinavyohitajika ili kuendeleza shughuli zake.
Soma zaidi: Hali ya kibinaadamu yazidi kuwa mbaya Gaza
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Operesheni za shirika hilo, Pascal Hundt, ameeleza kuwa wakaazi wa Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na hali mbaya na mapambano ya kila siku ili kujinusuru na hatari za mapigano, kuhamishwa kwa lazima na kunyimwa misaada ya kiutu inayohitajika haraka.