SiasaAsia
Urusi yautambua rasmi utawala wa Taliban
4 Julai 2025Matangazo
Tangazo hilo limewekwa wazi muda mfupi baada ya Muttaqi kukutana na balozi wa Urusi Dmitry Zhirnov, mjini Kabul. Zaidi kuhusu uamuzi huo Muttaqi amenukuliwa akisema kuwa, "Tumewapeleka wanadiplomasia wetu kwenye mataifa ambayo tuna mabalozi wetu, pili, nchi hizo zimewakubali mabalozi wetu ikiwemo Urusi. Urusi imekuwa ya kwanza kututambua na tuna matumaini mwenendo huu utaendelea. Tunalipongeza hili, ni hatua kubwa na itaimarisha zaidi uhusiano wetu na Urusi.
Nchi hizo zinatazamia kushirikiana kuimarisha usalama, kupambana na ugaidi pamoja na ulanguzi wa dawa za kulevya.