MigogoroJamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
MONUSCO yasema makumi ya Wakongo wameuawa na waasi wa ADF
19 Agosti 2025Matangazo
Taarifa ya Ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Kongo, MONUSCO, imesema mashambulizi hayo ya ADF yalitokea kati ya Agosti 9 hadi 16 kwenye maeneo ya Beni na Lubero yaliyopo katika jimbo la Kivu Kaskazini.
Maeneo hayo tayari yanakabiliwa na hali mbaya ya kiutu kutokana na mzozo wa miaka mingi unaoendelea mashariki mwa Kongo.
MONUSCO imesema hujuma hizo zimeshuhudia pia vitendo vya utekaji nyara, uporaji mali na uharibifu mwingine ikiwemo kuchomwa moto nyumba, magari na pikipiki.
Mamlaka za Kongo zimesema waasi hao wa ADF pia wanahusika na mauaji ya watu wapatao 40 kwenye jimbo la Ituri yaliyotokea mwezi uliopita.