SiasaAsia
Modi asema Trump hakuwa mpatanishi kati ya India na Pakistan
18 Juni 2025Matangazo
Mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa India, Vikram Misri, amesema Jumatano kuwa viongozi hao wawili walizungumza kwa njia ya simu, baada ya Trump kuondoka mapema katika mkutano wa kilele wa viongozi wa kundi la mataifa saba yaliyoendelea kiuchumi duniani ya G7.
Misri amesema Modi alimueleza wazi Trump kwamba katika mazungumzo yaliyofanyika, hapakuwa na mjadala wowote, katika ngazi yoyote, kuhusu mkataba wa biashara kati ya India na Marekani au pendekezo lolote la upatanishi wa Marekani kati ya India na Pakistan.
Awali, Trump alisema kuwa India na Pakistan zilikubaliana kuumaliza mzozo wa siku nne Mei 10, baada ya mazungumzo marefu yaliyosimamiwa na Marekani.