JamiiIsrael
Mmoja afa kwenye shambulizi huko Haifa, Israel
3 Machi 2025Matangazo
Taarifa iliyotolewa na ofisi ya msaada wa dharura nchini humo imesema mwanaume mwenye umri wa miaka 70 aliyejeruhiwa kwenye shambulizi hilo amekufa na majeruhi wengine wawili wako kwenye hali mahututi.
Mashuhuda wav mkasa huo wamesema mwanaume mwenye kisu na bunduki aliwashambulia watu ovyo alfajiri ya leo kwenye mji wa Haifa.
Inaarifiwa kwa jumla amewajeruhi watu wasiopungua 6 na duru zinasema maafisa wa usalama "wamemuua mshambuliaji huyo".