Mkutano kuhusu taifa la Palestina kufanyika Septemba
16 Julai 2025Matangazo
Chanzo hicho kimesema kuwa mkutano huo utakuwa wa ngazi ya mawaziri na utatafuta kuendeleza juhudi za utambuzi wa taifa la Palestina kwa mataifa kadhaa ambayo bado hayajaitambua, ikiwa ni pamoja na Ufaransa.
Pia kimeeleza kuwa mkutano huo utazingatia kurudisha uhusiano wa kawaida na ushirikiano na mataifa ya Kiarabu na Kiislamu.
Guterres ahimiza juhudi zaidi kutimiza ahadi ya suluhisho la mataifa mawili
Chanzo hicho kimesema kuwa wakuu wa nchi na serikali baadaye watakutana aidha Paris ama New York, kabla ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ambalo litahudhuriwa na viongozi wa dunia mnamo Septemba 22.
Wizara ya mambo ya nje ya Ufaransa imesema waziri wa mambo ya nje Jean-Noel Barrot atahudhuria mkutano huo.