Mjumbe maalum wa Urusi kukutana na mwenzake wa Marekani
2 Aprili 2025Matangazo
Kiril Dmitriev, ambaye ni mkuu wa hazina ya fedha za kigeni ya Urusi, aliyeteuliwa mwezi uliopita kuwa mjumbe maalum kwenye masuala ya uchumi wa kimataifa na ushirikiano wa uwekezaji, atakutana na mjumbe maalum wa Marekani, Steve Witkoff, kwa mujibu wa vyanzo hivyo.
Dmitriev na Witkoff wanatazamiwa kuzungumzia njia za kuimarisha uhusiano wa nchi zao, wakati huo wakisaka njia ya kukomesha vita nchini Ukraine.
Ziara ya Dmitriev ni ya kwanza kufanywa na afisa wa ngazi za juu wa Urusi mjini Washington, tangu Urusi ilipoivamia Ukraine mwaka 2022.