Mike Tyson na Floyd Mayweather kukutana ulingoni 2026
5 Septemba 2025Matangazo
Kampuni ya yenye kujihusisha na mchezo wa masumbwi, CSI Sports, imetangaza pambano hilo kati ya Tyson, ambaye atatimiza miaka 60 mwaka ujao, na Mayweather mwenye umri wa miaka 48. Hata hivyo, haijatoa maelezo kuhusu mahali pambano litakapofanyika wala tarehe rasmi. Tyson, bingwa wa zamani wa uzito wa juu duniani, alishindwa kwa pointi dhidi ya Jake Paul katika pambano la raundi nane lililofanyika Novemba 2024. Floyd Mayweather alitwaa mataji ya dunia katika aina tano ya viwango vya uzito tofauti, na hakuwahi kushindwa katika mapambano yake 50. Alihitimisha mchezo huo 2017 kwa ushindi dhidi bondia maarufu, Conor McGregor.