JangaPakistan
Miili zaidi yapatikana janga la mafuriko Pakistan
18 Agosti 2025Matangazo
Hadi sasa karibu watu 300 wamekufa kutokana na janga hilo lililotokea katika wilaya ya Buner.
Wakaazi wa vijiji vya wilaya hiyo wanasema watu wengine kadhaa bado hawajapatikana na juhudi za kuwatafuta zimeelekezwa kwenye vifusi vya majengo yaliyoanguka kutokana na maji mengi ya mafuriko yaliyotitirika kutoka maeneo ya milima.
Mafuriko hayo yamesababishwa na mvua kubwa za masika ambazo pia zimeleta maafa ikiwemo vifo katika jimbo linalozozaniwa baina ya India na Pakistan la Kashmir